1. Vishazi tegemezi virejeshi

Ni vishazi vinavyotumia virejeshi ‘-amba’ au ‘o’ ili kuvumisha nomino

kwa mfano: Gari ambalo lilinunuliwa litauzwa sokoni kesho

                    mto uliofurika mwaka jana ulitatiza wasafiri sana

  1. Vishazi tegemezi vya masharti 

Ni vishazi ambavyo huonyesha dhana ya utegemezi kwa kutumia viambishi ‘-nge-’, ‘-ngali-’,’-ngeli-’ na ‘ki’ na aghalabu hutumia viunganishi ya masharti kama vile ‘kiwa’ endapo, na iwapo   kwa mfano: 

 Ukisoma kwa bidii urafaulu maishani.

  Ikiwa nitampata maria mitamwambia

  Angelisoma kwa bidii angelipita mtihani.

  1. Vishazi tegemezi vya kuonyesha kinyume au kasoro

Hivi ni vishazi ambavyo hutumia viunganishi vya kuonyesha kinyume

K.m vile licha ya, japo,ijapo,ijapokuwa n.k.

k.m. Alimwadhibu ingawa hakuwa na makosa.

Ingawa mshahara wake si mkubwa anaikimu familia yake

  1. Vishazi tegemezi vya kuonyesha sababu

Huundwa kwa viunganishi vya sababu kama vile; kwa sababu, kwa kuwa, kwa vile

kwa mfano; Alikimbia shuline kwa sababu alikuwa amechelewa

                      Alitembea kwa miguu kwa kuwa  kulikuwa na uhaba wa magari

  1. Vishazi tegemezi vya wakati

Vishazi hivi huonyesha wakati wa kutendeka kwa jambo na hutumia vihusishi vya wakati kama vile;  tangu, baada ya, kabla ya na kiambishi ‘po’

kwa mfano;

Tulipoingia kwake alitukaribisha kwa furaha

Alisalimu amri baada ya kuvumaniwa na walinda usalama

  1. Vishazi tegemezi vya namna au jinsi

Huonyesha namna kitendo kilivyofanyika na hutumia kirejeshi ‘o’

kwa mfano:

Ulivyokuwa ukicheza jana ulitufurahisha

ulivyokuwa unakula jana ulituogofya

  1. Vishazi tegemezi vya mahali

huonyesha mahali ambapo kitendo kilitendeka . vishazi katika karegoria hii hutumia viambishi PO-KO-MO

 kwa mfano:

Alikosomea  ninapajua

Alimoingia napajua vizuri

  1. Vishazi Viambata

Ni vishazi vinavyoundwa kwa vishazi huru viwili vikiwa vimeunganishwa k.m. Baba analala na mama anapika.

 Vishazi tegemezi vipo vya aina mbili kutokana na majukumu yake kimuundo

A.    Kishazi tegemezi kivumishi (V)

Kishazi tegemezi kivumishi hufanya kazi ya kuvumisha nomino katika tungo.

      Mfano;            Baba anayenijali

                              Mbwa aliyepotea

                              Mwanafunzi aliyefariki

                              Uliyemuona pale

                              Aliyempenda sana

B.     Kishazi tegemezi kielezi (E)

 Kishazi hiki hufanya kazi ya kueleza tendo katika tungo na hujitokeza kueleza dhima tofauti tofauti kama ifuatavyo:-

  •  Kueleza mahali tendo linapofanyika. Mfano; Alipoingia (mahali dhahiri), Alimochungulia (ndani ya kitu Fulani), Alikoelekea (mahali pasipo dhahiri)
  •  Kueleza wakati wa tendo. Mfano; Tulipotoka, Alipomchapa, Walipomsema n.k.
  •  Kueleza masharti katika tendo. Mfano; Akirudi, Angekuja, Angelimpiga, Angalijua n.k.
  •  Kueleza namna tendo linavyofanyika. Mfano; Alivyoimba, Walivyopendeza, Tulivyomsifu.
  • Kueleza kasoro katika kukamilisha tendo. Mfano; Ingawa amesoma, Licha ya kufaulu, Japokua amependekezwa.
  •  Kueleza sababu ya kufanyika kwa tendo. Mfano; Kwa sababu alipendeza, Kwa kuwa hujafaulu, Kwa vile umenisomesha.

Zoezi

        Bainisha Vishazi Katika Sentensi Zifuatazo

  1. Mwalimu amewasili.
  2. Amina ambaye ni daktari atakuja.
  3. Ametajirika japo hakupata elimu.
  4. Mwalimu anafundisha na wanafunzi wanaandika.
  5. Tumeanzisha shirika ili tunyanyue hali zetu.
Kishazi
Kishazi huru
Kishazi tegemezi
Sifa za Kishazi tegemezi