AINA ZA SILABI

 Kuna wananadharia wanaosema kuwa silabi inaweza kuwasilishwa kwa namna mbalimbali. Pike na Pike (1943) wanasema kuwa muundo wa silabi una matawi na darajia. Baadhi ya wanataaluma wanaona kuwa silabi ina mwanzo na kilele. Wengine hudai kuwa silabi ina upeo na ukingo/mpaka/margin (sehemu ya mwanzo au ya mwisho wa silabi. Kuna wanazuoni wengine kama vile Halle, Harris na Vernaud wanasema kuwa silabi ina vitamkwa vinavyobeba sifa bainifu. Aidha, silabi zenye matawi na darajia zina tia.

Katamba (1996:176) anasema kuwa suala la kuainisha silabi kwa vigezo huru na funge ni la kimapokeo ama kijadi. Hivyo basi tunatakiwa kuangalia silabi husika kama ni nzito au nyepesi.

SILABI NZITO

Ni ile silabi ambayo upeo wake una tawi linalogawanyika.

Kwa mfano;

Mwanzo wa silabi                                                                       upeo wa silabi ah

l

                                                                        Kiini cha silabi                        ukingo wa silabi

                                                                               a                                                     h

SILABI NYEPESI

Ni ile silabi ambayo upeo wake haugawanyiki kwa mfano ba, ma da ,fa ja n.k.

                                                                                    6

                                       Mwanzo wa silabi                            upeo wa silabi

                                                   M                                               a

Mwanzo wa silabi ndio una msukumo wa matamshi. Hivyo basi silabi ma ni huru ni ni nyepesi kwani haina tawi linalogawanyika.

Kila lugha ina muundo wake wa silabi kulingana na idadi ya fonimu zilizopo.

MUUNDO WA SILABI HURU ZA KISWAHILI

Muundo wa irabu pekee kwa mfano katika ua, oa, au

Muundo wa nazali pekee kwa mfano katika mganga, mtoto, mdogo

Muundo wa konsonanti na irabu kwa mfano katika kaka, dada, debe, baba, raha

Muundo wa konsonanti konsonanti na irabu kwa mfano

(a)    Kipasuo+kiyeyusho+irabu kwa mfano, pweke

(b)   Kikwamizo+kiyeyusho+irabu kwa mfano, swaga

(c)    King’ong’o|+kiyeyusho+irabu kwa mfano. Mwaka

(d)   Kikwamizo+kipasuo+irabu kwa mfano spika

(e)    Kipasuo+kiyeyusho+irabu kwa mfano, bweka

Konsonanti konsonanti kiyeyusho na irabu kwa mfano;

(a)    Nazali+kipasuo+kiyeyusho+irabu kwa mfano pingwa

(b)    Nazali +kipasuo+ kiyeyusho+irabu kwa mfano pandwa, undwa

(c)    Nazali+ kikwamizo+kiyeyusho+irabu kwa mfano chinjwa

MUUNDO WA SILABI FUNGE

Aina hizi za silabi haziishii na irabu. Pia huwa hazisikiki na huweza kutokea mwanzoni, katikati au mwishoni mwa neno

MWANZONI MWA NENO

1.      Silabi zenye ukingo /l/ kwa mfano

Alfajiri, almasi, halmashauri, hulka n.k.

2.      Silabi zenye ukingo /s/ kwa mfano

Askari, askofu, desturi, mustarehe, rasmi, hospital, taslimu, wastani n.k.

3.      Silabi zenye ukingo /k/ kwa mfano

Daktari, bakshishi, iktisadi, takribani, aksante, maksai, muktadha, nuksi, nukta n.k.

4.      Silabi zenye ukiongo /r/ kwa mfano

Ardhi, karne n.k.

5.      Silabi zenye ukingo /n/ kwa mfano

Ankra

6.      Silabi zenye ukingo /m/ kwa mfano

Hamsini, mamsapu, alhamudullilah, hamsa n.k.

7.      Silabi zenye ukingo /p/ kwa mfano

Aprili, kaptula, kapteni

8.      Silabi zenye ukingo /b/ kwa mfano

Biblia, kabla, rabsha n.k.

9.      Silabi zenye ukingo /j/ kwa mfano;

Majhununi

SILABI ZENYE UKINGO ZINAZOTOKEA KATIKATI YA NENO

Kwa mfano, mfalme, daftari, eropleni n.k.

SILABI ZENYE UKINGO ZINAZOTOKEA MWISHONI MWA NENO

Kwa mfano jehanam, inshallah n.k.

Kwa ujumla maneno mengi yanayotumia silabi funge mengi ni ya kukopa.

DHIMA YA SILABI

–          Silabi ni kipashio cha msingi ambacho kina dhima ya kifonotaktiki (kanuni ambayo inamruhusu mzungumzaji kutumia mfuatano unaokubalika na kumkataza mfuatano usiokubalika. Kwa mfano, katika Kiswahili hakuna silabi inayoundwa kwa mfuatano kappa. Hivyo basi, muundo wa silabi hutusaidia kujua mfuatano sahihi kulingana na lugha husika.

–          Silabi inatumika kama mawanda ya kanuni za kifonolojia.

–          Silabi ni kama muundo wa kipande sauti changamano. Silabi hupambanua/hudhibiti mfuatano wa sifa thabiti.

–          Silabi ni kipashio ambacho hutumika kuunda vipashio vikubwa zaidi katika taaluma ya fonolojia kama vile toni, shada/mkazo. Pia inatumika kubainisha maana ya kifonolojia, kwa mfano, katika lugha ya Kiswahili tunaweka mkazo katika silabi ya pili kutoka mwisho wa neno.

hati miliki zimehifadhiwa

Leave a Reply

scroll to top