Ala za matamshi ni viungo vya mwili wa binadamu vinavyotumiwa kutamkia sauti kwa njia moja au nyingine wakati wa kuongea.Kuna aina mbili kuu ya za ala za matamshi;

a) Ala tuli

b) Ala sogezi

Ala tuli/ ala pahala

    Ni ala ambazo hazisogei  wakati wa kutamka sauti. Ala hizi ni kama vile   meno, ufizi, kaa kaa gumu, kaa kaa laini na koo/koromeo.

    Ala sogezi

    Ni ala ambazo husogea wakati wa kutamka sauti kama vile midomo na ulimi.

    Mchoro wa ala za matamshi

      Majina ya Ala za matamshi

      1. midodmo ya juu
      2. Midomo ya chini
      3. Meno ya juu
      4. Meno ya chini
      5. Ufizi/masine
      6. Kaakaa gumu
      7. Kaakaa laini
      8. Chemba cha pua/ mkondo wa hewa pua
      9. Chemba cha Kinywa /Mkondo wa hewa kinywa
      10. Ulimi
      11. Ncha ya ulimi
      12. Bapa la uimi
      13. Shina la ulimi
      14. Kidaka tonge
      15. Nyuzi za sauti
      16. Koo/Umio wa hewa/Koromeo/ Zoloto