Alama ya Kistari Kifupi (-)

1. Kistari kifupi hutumiwa Kuunganisha maneno mawili

Askari-Jeshi watashika doria katika msitu wa shakahola.

Nawatuma kama wana-kondoo miongoni mwa mbwa-mwitu.

2. Kistari kifupi hutumiwa Kuonyesha hadi, au mpaka

Bei ya mafuta imepanda kutoka shilingi 160 – 180

Tutasoma Bibilia kitabu cha Marko 4: 3 – 9

3. Kama alama ya kupunguza au kutoa katika Hesabu

17 – 7 = 10

10 – 5 = 5

4. Kistari kifupi pia huonyesha neno ambalo halijakamilika litaendelezwa katika msitari ufuatao

Mwalimu alisafiri kutoka ulaya kuja kuwa-

tembelea wazazi wake baada ya miaka kumi.

5. Kuonyesha tarehe

Muhula wa tatu utaanza 28-08-2023.

Wanafunzi watafungua shule tarehe 04-02-2014

ALAMA ZA UAKIFISHA
Alama za usemi(“”)
Dukuduku (…)
Koma/mkato/kipumuo( , )
Ritifaa/kibainishi( ’ )
Mshazari/mkwaju(/)
Kistari kirefu
Mstari( ___  )
Kikomo/kitone/nukta (.)
Nusu/semi koloni/nukta na kituo (;)
Vifungo/mabano/paradesi( )
Herufi kubwa(H)
Herufi ndogo (h)
Koloni/ Nukta mbili ( : )
Hisi/mshangao (!)
Herufi nzito (h)
Herufi za mlazo/italiki(h)
Kinyota(*)
Swali/Kiulizo

Leave a Reply

scroll to top