Alama ya Nukta-Mbili au Koloni (:)

1. Alama ya nukta mbili au koloni hutanguliza orodha:

Sherehe ya mama Maria ilihudhuriwa na watu wa wengi: wake kwa waume; wadogo kwa wakubwa; wazee kwa vijana.

Kuna aina kadhaa ya viwakilishi: Viwakilishi vya sifa, viwakilishi vya idadi, viwakilishi vya mahali n.k.

2. Koloni pia huelezea sababu au kuonyesha matokeo ya kitu.

Karanja alipoingia darasani alipigwa na butwaa: rafikiye Joshua alikuwa amezimia.

Koome alinipatia zawadi nzuri sana: nilirukaruka kwa furaha.

3. Koloni vilevile hutenga saa na madakika Kwa mfano:

Wanafunzi waliingia darasani 3:15.

Walifika uwanja ndege 6:45

4. Koloni hutumiwa pia Kunukuu ukurasa wa Bibilia

Mchungaji alisoma kitabu cha Luka 5:4-9

Katika kitabu chaYohana 8: 6-11, Bibilia inasema…

5. Koloni pia hutumiwaKuonyesha maneno ya msemaji katika tamthilia au mchezo wa kuigiza

Mwelusi: Unafikiria mimi ni mtu wa kuchezewa?

Sudi: (akitetemeka) Tafadhali naomba unisamehe.

6. Koloni pia huonyesha mada katika barua au kumbukumbu za mkutano

KUH: Ombi Lakuomba kazi yaUseremala

KUH: Barua ya tarehe 6/4/2009.KUM: 2/321/2020 Mbinu Mpya za Kunyamazisha Raia

7. Koloni hutumiwa Katika kumbukumbu za mkutano

KUM 2/321/2000: Mbinu mpya za kunyamazisha raia.

Ajenda 2: Kusomwa kwa kumbukumbu za mkutano uliotangulia.

ALAMA ZA UAKIFISHA
Alama za usemi(“”)
Dukuduku (…)
Koma/mkato/kipumuo( , )
Ritifaa/kibainishi( ’ )
Mshazari/mkwaju(/)
Kistari kifupi( – )
Kistari kirefu
Mstari( ___  )
Kikomo/kitone/nukta (.)
Nusu/semi koloni/nukta na kituo (;)
Vifungo/mabano/paradesi( )
Herufi kubwa(H)
Herufi ndogo (h)
Hisi/mshangao (!)
Herufi nzito (h)
Herufi za mlazo/italiki(h)
Kinyota(*)
Swali/Kiulizo

Leave a Reply

scroll to top