CHANGAMOTO/MAPUNGUFU KATIKA UKALIMANI NA TAFSIRI

 Mfasiri katika kazi yake ya kufasiri hukumbana na changamoto mbalimbali, ambazo huweza kusababisha tafsiri kuwa na mapungufu ya hapa na pale. Baadhi ya changamoto au mapungufu hayo ni kama vile:

(i) Tofauti za kiisimu kati ya lugha chanzi na lugha lengwa.

Tofautui za maumbo, miundo na maana kati ya lugha ya Kiswahili na lugha ya Kingereza wakati mwingine husababisha matatizo au upungufu katika tafsiri na ukalimani. Kwa mfano maumbo ya vitenzi vya Kiingereza huruhusu kauli nyingi elekezi kutoonesha umoja au wingi wa wahusika wala majina ya vitu mahususi vinavyoambatana na maelekezo yanayotolewa tofauti maumbo ya vitenzi vya Kiswahili ambavyo huonesha umoja na wingi wa wahusika na hata kuwa na majina ya vitu husika, tazama mifano ifuatayo kama ilivyotolewa na, Mwansoko [2006]

Kingereza Kiswahili

No parking ? Usiegeshe gari hapa [je kisichoruhusiwa kuegeshwa ni gari tu?]

No Smoking ? Usivute sigara[ Je ni sigara tundiyo hairuhusiwi kuvutwa?]

Arrivals ? Wanaowasili

Departures ? Wanaosafiri

Vilevile tofauti za maana kati ya lugha ya Kingereza na Kiswahili huweza kuathiri tafsiri au ukalimani, mathalani:

Kiswahili Kingereza

Wasiojiweza ? Disabled [Siyo wote wasiojiweza ni walemavu]

[na siyo walimavu wote hawajiwezi]

Wezi wa mifukoni? Pickpockets [Hawaibi kwenye mifuko, wanaiba kutoka mifukoni]

(ii) Tofauti za mitindo kati lugha chanzi na lugha lengwa

Tofauti za mitindo ya uzungumzaji pia, huweza kuathiri tafsiri na ukalimani na hii ni kwa sababu unaweza kukuta kuna mitindo fulani inaweza kutumika katika muktadha fulani lakini ikishindwa kupata tafsiri katika lugha nyingine katika muktadha ule ule.mathalani:

Kingereza: Kiswahili

(i) Thou shalt not steal [mtindo wa kidini] ? Usiibe

Do not steal [mtindo wa kawaida] ? Usiibe

(ii) Lend me your ears [mtindo wa kishairi] ? Naomba mnisikilize

May I have your attention [kawaida] ? Naomba mnisikilize

Tafsiri zote tulizoziangalia katika mfano wa (i) na (ii) zimetoa maana au taarifa ili ile iliyomo katika matini chanzi lakini tafsiri hizo hazikuzingatia mtindo wa lugha iliyotumika katika matini chanzi.

(iii) Tofauti za kitamaduni kati ya lugha chanzi na lugha lengwa

Tofauti za kiutamaduni, yaani taofauti za kimila, desturi na mazingira ya watumiaji wa lugha chanzi na lugha lengwa huweza kufanya tafsiri au ukalimani kuwa mgumu, kwa mfano, katika utamaduni wa Waingereza wana milo minne wakati Waswahili wana milo mitatu na hii hupelekea kuwa vigumu kupata dhana za milo ya hiyo ya Waingereza katika dhana ya Kiswahili. Mfano:

Waingereza wana: Waswahili wana:

Breakfast —————— Kifungua kinywa

Lunch …………………… Chakula cha mchana

High tea ……………………?

Dinner ……………………Chakula cha jioni

Supper …………………….?

Kwa hiyo ukiangalia mifano hiyo, utaona kuwa, high tea na supper kuzipata dhana zake katika lugha ya Kiswahili ni ngumu kutokana na kutokuwa na utamaduni wa kuwa na milo kama hiyo kwa siku. Lakini pia inakuwa vigumu kupata tafsiri ya vyakula kama vile ugali, makande katika lugha ya Kiingereza kutokana na kutokuwa na vyakula vya aina hiyo.

(iv) Tofauti za kiitikadi kati ya lugha chanzi na lugha lengwa

Tofauti za kiitikadi pia huweza kuathiri tafsiri na ukalimani, na hii ni kwa sababu, utakuta wafasiri wengi hususani waandishi wa habari kuegemea katika itikadi zaidi, kwa mfano:

Kingereza Kiswahili

Bussnessman ? mlanguzi [tafsiri hii inatokana mfasiri kuathiriwa na itikadi

ya ujamaa]

mfanyabiashara [tafsiri hii inatokana mfasiri kuathiriwa na

itikadi ya ubepari]

Freedom fighter ? wapigania uhuru [Tafsiri ya vyombo vya habari vya

Tanzania wakati wa kupigania uhuru]

Magaidi [Tafsiri ya idhaa ya BBC na Radio za Afrika

Kusini wakati huo]

Hivyo basi kwa kuhitimisha tunaweza kusema kuwa, ukalimani mzuri unawezekana kwa kiwango ambacho mila na desturi zote yaana za lugha chanzi na lugha lengwa zinalingana ama kushabihiana.

Na kutokana na umuhimu wa taaluma hii ya tafsiri na ukalimani, serikali kupitia Baraza la Kiswahili la Taifa Bakita [BAKITA] imeanzisha idara maalumu ya Tafsiri na Ukalimani, na idara hiyo ina majukumu yafuatayo:

  • Kutoa huduma za tafsiri na ukalimani kwa lugha mbalimbali kwa masharika, idara, wizara, balozi na watu binafsi.
  •  Kuratibu na kutoa huduma za ukalimani kwenye mikutano ya kitaifa na kimataifa na katika shughuli za masharika, makampuni na watu binafsi.
  • Kupitia na kuthibitisha tafsiri zilizofanywa na asasi mbalimbali au wafasiri wa nje.
  • Kutoa ushauri kuhusu masula ya tafsiri na ukalimani.

MAREJEO

Cartford [1995] A linguistic Theory Translation

Mwansoko, H.J.M na wenzake [2006] Kitangulizi cha Tafsiri, Nadharia na

Mbinu.TUKI.Dar-es-salaam

Newmark, P [1982] Approaches to Translation, Oxford, Pergamon Press

Newmark, P [1988] A Text book of Translation, London, Prentice Hall.

Oxford University Press Dar-es-salaam

Semzaba, E [2006] Ngoswe, Penzi Kitovu cha Uzembe. The General Booksellers LTD.

D.S.M

TUKI [2002] Kamusi ya Kiswahili Sanifu. TUKI, Dar-es-salaam

TUKI [1985] Kiswahili, Jarida la Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili.

www.bakita.org.tz retrieved on Monday 04th July 2018

www.jim-mission.org.uk retrieved on Monday, 04th July 2018

www.ajol.inf retrieved on Monday, 04th July 2018

Vitabu vilivyotafsiriwa ambavyo vimetumika kama marejeo

Ayi Kwei Armah, Wema Hawajazaliwa, kimetafsiriwa na Abdilatif Abdalla

Ferdinand Oyono: House boy, Kimetafsiriwa na Raphael Khasao na Nathan Mwele.

William Shakespeare: Juliasi Kaizari: Kimetafsiria na Julius K. Nyerere

Mabepari wa Venisi: Kimetafsiriwa na Julius K. Nyerere

Hekaya za Abunuwasi: Kimetafsiriwa na Interterritorial Language Committee, East Africa

Alfu Lela Ulela: Kimetafsiriwa na Sir Richard Burton

Sir Rider Haggard: Mashimo ya Mfalme Suleiman


hati miliki zimehifadhiwa

Leave a Reply

scroll to top