DHIMA ZA TAFSIRI NA UKALIMANI

 Tafsiri na Ukalimani ina dhima zifuatazo:

  • Hutuwezesha kujifunza lugha tofauti.

Kati ya mazoezi mazuri anayoweza kutumia mtu katika kujifunza lugha nyingine, basi zoezi la kutafsiri au kukalimani mara kwa mara humsaidia mtu kujifunza lugha kwa urahisi zaidi, kwani kwa kufanya tafsiri ya mara kwa mara kutamsaidia mtu kugundua miundo na vipengele mbalimbali vya lugha na jinsi vinavyofanya kazi katika lugha anayojifunza.

  • Hutumika kama njia ya mawasiliano.

Kutokana na maingiliano ya mataifa mbalimbali yanayotumia lugha tofauti tofauti, tafsiri hutumika kurahisisha mawasiliano baina ya makundi ya watu wanaotumia lugha tofauti tofauti, hutumika kutolea maelezo ya kibiashara kama vile maelekezo ya jinsi ya kutumia bidhaa mbalimbali zinazozalishwa nje au zinazouzwa nje ya nchi, katika matangazo ya kitalii ili kuwavutia watalii kutoka mataifa mbalimbali, vilevile hutumika katika vyombo vya habari, tafsiri pia inatumika katika nyaraka rasmi, mikataba, vitabu vya ziada na kiada, lakini pia ukalimani hulahisisha mawasiliano miongoni mwa watu wanaozungumza lugha tofauti.

  • Tafsiri na Ukalimani hutumika kueneza utamaduni.

Tafsiri imekutanisha lugha na tamaduni mbalimbali duniani na kusababisha tamaduni na lugha hizo kuathiriana, kwa mfano mara baada ya waarabu kuingia Afrika Mashariki na vitabu mbalimbali vya Kiarabu na Kiislamu kutafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili ilisababisha utamaduni wa Kiswahili kuathiriwa na utamaduni wa Kiarabu na Kiislamu kutoka na kuiga kwa mambo mengi kutoka huko, lakini pia hata walipokuja wazungu na kutafsiri vitabu vyao vya kifasihi, kutafsiriwa kwa Biblia, n.k. ilisababisha pia utamaduni wa Mswahili kuathiriwa na utamaduni wa Ulaya.

  • Tafsiri na Ukalimani ina dhima ya kuwasilisha ujumbe wa manufaa kwa watu ambao hawafahamu lugha chanzi [lugha asilia]

MAREJEO

Cartford [1995] A linguistic Theory Translation

Mwansoko, H.J.M na wenzake [2006] Kitangulizi cha Tafsiri, Nadharia na

Mbinu.TUKI.Dar-es-salaam

Newmark, P [1982] Approaches to Translation, Oxford, Pergamon Press

Newmark, P [1988] A Text book of Translation, London, Prentice Hall.

Oxford University Press Dar-es-salaam

Semzaba, E [2006] Ngoswe, Penzi Kitovu cha Uzembe. The General Booksellers LTD.

D.S.M

TUKI [2002] Kamusi ya Kiswahili Sanifu. TUKI, Dar-es-salaam

TUKI [1985] Kiswahili, Jarida la Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili.

www.bakita.org.tz retrieved on Monday 04th July 2018

www.jim-mission.org.uk retrieved on Monday, 04th July 2018

www.ajol.inf retrieved on Monday, 04th July 2018

Vitabu vilivyotafsiriwa ambavyo vimetumika kama marejeo

Ayi Kwei Armah, Wema Hawajazaliwa, kimetafsiriwa na Abdilatif Abdalla

Ferdinand Oyono: House boy, Kimetafsiriwa na Raphael Khasao na Nathan Mwele.

William Shakespeare: Juliasi Kaizari: Kimetafsiria na Julius K. Nyerere

Mabepari wa Venisi: Kimetafsiriwa na Julius K. Nyerere

Hekaya za Abunuwasi: Kimetafsiriwa na Interterritorial Language Committee, East Africa

Alfu Lela Ulela: Kimetafsiriwa na Sir Richard Burton

Sir Rider Haggard: Mashimo ya Mfalme Suleiman


hati miliki zimehifadhiwa

Leave a Reply

scroll to top