Irabu ni sauti ambazo hutamkwa kwa ulaini bila hewa kuzuiliwa katika ala za sauti.

Irabu za kiswahili ni tano. Nazo ni /a/, /e/, /i /, /o/ , na /u/.kila irabu huwa na sifa zake

Uainishaji wa Irabu

ulimi ndicho kiungo muhimu  zaidi katika utamkaji wa irabu/vokali .ulimi huweza kukunjwa  kwa njia mbalimbali.

Irabu huanishwa kwa  kutegemea vigezo vitatu navyo ni:

  1.   Sehemu ya ulimi inayotumika kutamkia irabu husika  (Inaweza ikaw sehemu ya mbele au sehemu ya nyuma ya ulimi)
  2.   Muinuko wa ulimi katika kinywa ( ulimi unaweza ukawa chini, katikati au sehemu ya juu katika kinywa)
  3.   Mkao wa midomo ( midomo inaweza kuwa imeviringwa au kutandazwa) 

Kutokana na vigezo hivi irabi hizi tano za kimsingi huwa na sifa zifuatazo ambazo zinatokana na umbo lifuatalo:

Sifa za irabu

  1. /a/ ni Irabu ya katikati na chini kinywani na midomo ikiwa imetandazwa.
  2. /e/ ni ya mbele na kati kinywani na midomo ikiwa imetandazwa.
  3. /i/ ni irabu ya mbele na juu kinywani na midomo ikiwa imetandazwa.
  4. /o/ ni irabu  ya nyuma na kati kinywani na midomo ikiwa imeviringa.
  5. /u/ ni irabu ya nyuma na juu kinywani na midomo ikiwa imeviringa.

Tazama Jedwali Lifuatalo:

IrabuSehemu ya Ulimi ya KutamkiaMwinuko wa UlimiMkao wa midomo
/a/katikatichinitandazwa
/e/mbelekatitandazwa
/i/mbelejuutandazwa
/o/nyumakativiringwa
/u/nyumajuuviringwa

        Zoezi

  1. Taja makundi mawili ya sauti za Kiswahili.
  2. Yatofautishe makundi ya sauti za Kiswahili uliyotaja katika (a)
  3. Toa mifano miwili miwili ya irabu ambazo hutamkwa:
  1. midomo ikiwa imeviringa
  2. midomo ikiwa imetandazwa
  1. Eleza jinsi irabu /e/ inavyotamkwa.
  2. Taja aina mbili za ala za kutamkia na utoe mfano mfano mmoja mmoja.