MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA UKALIMANI

 Kwa ujumla yapo mambo kadha wa kadha, ambayo mkalimani anatakiwa kuyazingatia anapotaka kufanya ukalimani, mambo hayo tunaweza kuyagawa katika makundi mawili, ambayo ni:

1. Kabla ya kuanza ukalimani

Katika hatua hii, mkalimani anatakiwa kuzingatia mambo yafuatayo:

(a) Awe na uelewa mzuri wa lugha zote anazotaka kukalimani, hapa tuna maana kuwa awe na uwezo wa kuzungumza na kuelewa lugha chanzi na lugha lengw, hii itasaidia mkalimani kutopotosha kile kinachozungumzwa na mzungumzaji wa lugha chanzi.

(b) Awe anaijua historia na utamaduni wa jamii zote mbili, yaani ile ya lugha chanzi na ile ya lugha lengwa.

(c) Kama ni ukalimani rasmi, ni vizuri kwa mkalimani akamjua mzungumzaji wa lugha chanzi, ni vema pia ukafanya naye mazungumzo kidogo ili kumzoea, na kutambua vionjo vyake ili iwe rahisi kwa mkalimani pindi atakapokuwa anafanya ukalimani asionekane kama mgeni.

(d) Vilevile ni muhimu kwa mtu anayekalimani, akawa na uelewa mzuri wa mada inayozungumzwa, hii itamrahisishia mkalimani katika ukalimani wake.

2. Katika ukalimani wenyewe

Mkalamani anapokuwa amesimama mbele ya hadhira [wasikilizaji] pamoja na mzungumzaji wa lugha chanzi kwa ajili ya kuanza ukalimani, anatakiwa kuzingatia mambo yafuatayo:

(a) Kuwa makini katika kusikiliza kile kinachozungumzwa na mzungumzaji wa lugha chanzi ili kuepuka kuachwa mahali na kuepuka kumuomba mzungumzaji kurudia mara kwa mara.

(b) Itambue hadhira ya lugha lengwa, ni watu wa namna gani, wana kiwango gani cha elimu, ni wasomi wa kawaida au waliobobea, ni watu wa jinsia na umri gani,? Hii itakusaidi kujua aina ya msamiati na miundo ya tungo utakayoitumia, kama iwe rahisi au migumu kutokana na hadhira yako ilivyo.

(c) Tumia mitindo unayodhani itaeleweka vema na hadhira/ wasikilizaji wa lugha lengwa, kwa mfano kama hadhira yako ni vijana, jaribu kutumia mitindo inayopendwa na vijana, kama wasikilizaji wako ni watu rasmi na we huna budi kuwa rasmi.

(d) Weka mkazo sehemu ambazo mzungumzaji wa lugha chanzi anaweka mkazo ili kuepuka utofauti yako na mzungumzaji wa lugha chanzi, na hata kuepuka kuathiri lengo la mzungumzaji wa lugha chanzi.

(e) Unatakiwa pia kutumia ishara zinazotumiwa na mzungumzaji wa lugha chanzi, hii itawafanya wasikilizaji waamini kile kinachozungumzwa na mzungumzaji wa lugha chanzi ndiyo kilekile kinachozungumzwa na mkalimani.

(f) Usiwe muda mwingi unamtazama mzungumzaji wa lugha chanzi na kusahahu kuitazama hadhira yako, hivyo unatakiwa kuitazama hadhira yako ili kugundua kama wako pamoja na wewe au kuna sehemu hawajakuelewa ili uweze kuwafafanulia zaidi.

(g) Muombe mzungumzaji wa lugha chanzi kurudia sehemu unayodhani hujaisikia au hujaielewa vizuri, kwani ni makosa kwa mkalimani kukalimani sehemu au jambo ambalo hukulisikia vizuri au kulielewa.

Hivyo basi hayo ndiyo mambo muhimu ambayo mkalimani anatakiwa kuyazingatia anapokuwa anafanya ukalimani. Jambo la kuzingatia, mkalimani hutakiwa kuingiza hisia zako unapokuwa anafanya ukalimani. na ukalimani mzuri unawezekana kwa kiwango ambacho mila na desturi zote yaani za lugha chanzi na lugha lengwa zinalingana ama kushabihiana.


MAREJEO

Cartford [1995] A linguistic Theory Translation

Mwansoko, H.J.M na wenzake [2006] Kitangulizi cha Tafsiri, Nadharia na

Mbinu.TUKI.Dar-es-salaam

Newmark, P [1982] Approaches to Translation, Oxford, Pergamon Press

Newmark, P [1988] A Text book of Translation, London, Prentice Hall.

Oxford University Press Dar-es-salaam

Semzaba, E [2006] Ngoswe, Penzi Kitovu cha Uzembe. The General Booksellers LTD.

D.S.M

TUKI [2002] Kamusi ya Kiswahili Sanifu. TUKI, Dar-es-salaam

TUKI [1985] Kiswahili, Jarida la Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili.

www.bakita.org.tz retrieved on Monday 04th July 2018

www.jim-mission.org.uk retrieved on Monday, 04th July 2018

www.ajol.inf retrieved on Monday, 04th July 2018

Vitabu vilivyotafsiriwa ambavyo vimetumika kama marejeo

Ayi Kwei Armah, Wema Hawajazaliwa, kimetafsiriwa na Abdilatif Abdalla

Ferdinand Oyono: House boy, Kimetafsiriwa na Raphael Khasao na Nathan Mwele.

William Shakespeare: Juliasi Kaizari: Kimetafsiria na Julius K. Nyerere

Mabepari wa Venisi: Kimetafsiriwa na Julius K. Nyerere

Hekaya za Abunuwasi: Kimetafsiriwa na Interterritorial Language Committee, East Africa

Alfu Lela Ulela: Kimetafsiriwa na Sir Richard Burton

Sir Rider Haggard: Mashimo ya Mfalme Suleiman


hati miliki zimehifadhiwa

Leave a Reply

scroll to top