MBINU ZA KUTAMBUA FONIMU NA ALOFONI ZAKE

 UTANGULIZI

Fonimu huchukuliwa kama kipashio kidogo zaidi cha sauti ambacho huweza kubainisha maana

katika maneno.kwa hivyo fonimu hapa huwa inakuwa foni inayotumikizwa katika lugha

mahususi.fonimu ndicho kipashio kidogo zaidi chenye kubainisha maana.fonimu huwa haina

maana kivyake lakini huchangia maana ya maneno.fonimu huwa na sifa ya ubainifu kwa sababu

hubainisha maana ya neno moja na linguine kwa mfano neno

i)Kanda na

tanda

sauti /k/ na /t/ katika (i) ndizo sauti zinazobainisha maana.sauti hizi basi ni sauti bainifu ambazo

ni fonimu.ubainifu huu hutokea kwa sababu tunapotumia sauti moja badala ya nyingine,maana

ya maneno au neno hubadilika.

Kwa upande mwingine alofoni ni matamshi mbalimbali ya fonimu moja au sura tofauti tofauti

za fonimu moja ambazo husababisha tofauti za maana.fonimu moja yaweza kutamkwa

kifonetiki kwa njia tofauti tofauti.Hutokea wakati ambapo fonimu moja inaweza kuwakilishwa

na zaidi ya sauti mbili zinazodhihirika kimatamshi,hizi tofauti za fonimu moja ndizo huitwa

alofoni.

Kwa mfano fonimu /a/ ya Kiswahili huwakilishwa na foni [ā] hata hivyo wakati mwingine /a/

huwakilishwa na vokali [ã] ya nasali.katika hali hii tunasema Kiswahili kina alofoni mbili za [ā]

yaani a kwa mfano katika neno mãmã na [ā]katika neno [sasa].

MBINU ZA KUTAMBUA FONIMU NA ALOFONI

a)mlingano wa kifonetiki

Hii ni dhana ambayo imezungumziwa na Hyman (1975) na Jones (1957) wanaelezea kuwa

alofoni za fonimu moja ambazo huonyesha mgawo wa kiutoano (hali ambayo sauti Fulani

hutokea katika mazingara Fulani na wala siyo mengine) lakini hazifanani kifonetiki haziwekwi

katika kundi moja.sauti zinazo fanana kifonetiki ni sauti zilizo na sifa bainifu zinazo fanana

Mgulu ( 2010 ) anaelezea kuwa kila lugha huteua baadhi ya sifa bainifu zinazotumiwa

kubainisha foni katika kiwango cha kifonetiki na wakazitumia katika kuzifafanua fonimu za

lugha yao.kulingana na Mweri(2010) anaeleza kuwa wakati mwingine hutokea hali ambapo

fonimu tofauti huonekana kama ambazo ni alofoni za fonimu moja.anatoa mfano wa kiingereza

akieleza kuwa sauti /ŋ/ na/h/huonekana kama ni alofoni za fonimu moja kwani/ŋ/ inapotokea

/h/haiwezi tokea.ansema kuwa hatuwezi kupata maneno yanayoishia kwa sauti /h/ katika

kiingereza,pia hakuna maneno yanayoanzia kwa sauti /ŋ/.kwa hali hii zinaonekana kama alofoni

za fonimu moja.kwa sababu sauti hizi zinakosa kufanana kifonetiki,fonimu hizi zinakua na sifa

zifuatazo;

-/h/ -isoguna

-Kikwamizi

– Glota

– Ya kinywa

/ŋ/ -guna

-kipasuo

-kaakaa laini

Ili sauti mbili ziwe alofoni za fonimu moja,ni sharti zifanane kifonetiki ili kuepukana na

uwezekano wa kuorodhesha sauti zozote kama alofoni za fonimu moja.

b)Mgawanyo wa kiutoano

katika mbinu hii,kitu ambacho kinazingatiwa ni ile hali ambayo sauti Fulani hutokea

katika mazingara Fulani na wala sio mengine.mbinu hii pia inatumika kubainisha sauti ambazo

ni fonimu au alofoni za lugha fulani.

R.S Mgulllu (2010) anaeleza kuwa fonolojia utoano ni dhana ambayo hutumiwa kuelezea

uhusiano uliopo baina ya sauti mbili za fonimu moja ambazo haziwezi kutokea katika mazingira

sawa,huku akimaanisha kuwa kila sauti ina mazingira yake maalumu ambayo hayawezi kukaliwa

na sauti nyingine.

Katika kitabu cha J.G Mweri (2010) utangulizi wa isimu. hali hii anaichukulia kama

mgawo kamilishani na kwa lugha ya Kiswahili anatupa mfano wa sauti/p/ ambayo inatamkwa

tofauti kutegemea na mazingara inamotokea anatoa mfano wa neno;

-/paka/

-/mpaka/

Katika maneno haya mawili,anasema kuwa neno /paka/ sauti /p/ hutamkwa na mpumuo

kidogo ilhali neno/mpaka /p/,hutamkwa bila mpumuo wowote. Aneleza kuwa mara nyingi /p/

inapotokea mwanzoni mwa neno au maneno katika Kiswahili hutamkwa na mpumuo,kwa

mfano neno [p h anya].na sauti hii inapotumika katika mazingara ya kati katika maneno

hutamkwa bila mpumuo wowote.anaelezea kuwa katika neno mpaka /p h /haiwezi kutokea

baada ya/m/.sauti /p/ na /p h / basi haziwezi kutokea katika mazingira sawa.

/p h /

P /p/ na /ph/ zinakua alofoni za fonimu moja ambayo ni[p]

/p/

c)Mpishano huru

mpishano huru ni hali mbayo sauti mbili zinaweza kutumika katika mazingira sawa bila ya

kubadilisha maana ya neno.kwa maneno mengine tunaweza kusema kuwa ni uhusiano wa

fonimu mbili tofauti kubadilishana nafasi moja katika maneno maalumu bila kubadili maana.

sauti hizi huwa tofauti kifonetiki na haziwezi kuwa alofoni za fonimu moja.sauti hizi

ambazo huwa tofauti kifonetiki huwa hazina ule uhusiano wa kiutoano,haziwezi kutumika

katika mazingira yale yale kwenye neno lakini sauti hizo ingawa ni tofauti hazisababishi tofauti

za maana katika maneno zinamotokea.

Kwa mfano; Angalau…………..angalao

Ramba…………….lamba

d)Jozi mlinganuo finyu

Jozi mlinganuo finyu ni mbinu ambayo inatumika kuzitambua fonimu za lugha. Mbinu

hii huwa ni hali ambayo maneno mawili katika lugha hutofautiana kwa sauti moja ambayo

hubainisha maana baina ya maneno hayo.sauti hizi huweza kutokea mwazoni mwa

maneno,katikati au hata mwishoni mwa maneno.kwa mfano;

-meno………………………neno

-kuni……………………….kumi

-kile………………………kila

Maneno ambayo yanahusika huwa lazima yawe na idadi sawa ya sauti na vile vile kila

neno ambalo linahusika liwe na mpangilio sawa wa sauti.katika hali hii basi ,ni kweli kusema

kuwa sauti mbili zinazo leta tofauti za kimaana katika maneno huwa ni kielelezo cha kifonetiki

cha fonimu mbili tofauti.

e)msawazisho changamano

Usawazisho hutokea pale ambapo sauti mbili tofauti katika lugha hupoteza tofauti zao hasa

katika mazingira Fulani katika neno.kwa mfano katika lugha ya Kiswahili usawazisho hujitokeza

katika neno ulimi.fonimu /l/ inatamkwa kama [d] inapotanguliwa na nazali ya ufizi /n/.kwa

hivyo neno hili ulimi(umoja) ndimi (wingi) /n/ hapa basi /l/ ndilo umbo

ndani na hubadilika katika mazingira inapotanguliwa na /n/ hali hii huwakilishwa kwa mchoro

hivi;

[l] [d]/n katika hali hii inamaanisha kuwa /l/ inageuka na kuwa

[d] katika umbo nje.

Marejeleo.

J.Habwe,P.karanja (2004)misingi ya sarufi ya Kiswahili phoenix publishers Ltd Nairobi.

J.Mweri (2010) utangulizi wa wa isimu

R.S Mgullu mtalaa wa isimu fonetiki,fonolojia na mofolojia ya Kiswahili Autolitho Ltd Nairobi.

hati miliki zimehifadhiwa

Leave a Reply

scroll to top