Miundo ya Kiima

Kiima ni neno au kifungu cha maneno katika sentensi ambacho hutangulia kitenzi na aghalabu huonyesha mtenda.Kiima huonyesha nomino au kiwakilishi ambacho hufanikisha kutendeka kwa kitendo.

Miundo ya kiima

Nomino pekee

Junet anapika ugali.

Ng’ombe anakula nyasi.

Cherop anasoma habari.

Nomino,kiunganishi na nomino

Duma na mbwa wemefungiwa pamoja.

Wanafunzi na walimu wanasoma magazeti.

Nomino na kivumishi

Mtoto yule  anapenda kandanda.

Datari huyo anatibu wagonjwa

Kiwakilishi

Hao wanaimba nyimbo za mapenzi.

Yule atasafiri kesho.

Kiwakilishi na kivumishi

Yule mtundu amefukuzwa shuleni.

Yale mengi yamevunwa.

Nomino na kishazi tegemezi

Muuguzi aliyewatubu wagonjwa jana amefutwa kazi.

Tanbihi: Kiima chaweza kutokea katika sehemu yoyote ya sentensi.

Leave a Reply

scroll to top