MKAZO

 MKAZO

Ni msisitizo / utamkaji wa silabi au neon kwa kutumia nguvu nyingi, hali ambayo huifanya silabi au neno hilo kusikika kuliko silabi nyingine katika neno husika au neno katika tungo.

AINA ZA MKAZO

(i)                 Mkazo mkuu

Huifanya silabi husika kusikika Zaidi kuliko silabi nyingine katika neno, kirai, kishazi au sentensi. Alama ᾽ ndiyo hutumika kuwalikisha mkazo huu.

(ii)               Mkazo wa kawaida

Hauna msikiko mkubwa kama mkazo mkuu ῝ ni alama itumikayo katika unukuzi wake.

Mkazo unaweza kutokea mwanzoni, katikati au mwishoni mwa neno. Kila lugha huwa na utaratibu wa uwekaji wa mkazo. Katika lugha ya Kiswahili mkazo huwekwa katika silabi ya pili kutoka mwisho wa neno.

hati miliki zimehifadhiwa

Leave a Reply

scroll to top