Mnyambuliko wa vitenzi

Kunyambua kitenzi ni kukiongeza viambishi tamati ili kukipa maana tofauti.

hubadilika kulingana na mnyambuliko wa kitenzi.

    KAULIKIAMBISHIMFANO
    KUTENDEAe, iomb-e-a, pig-i-a,
    KUTENDEANAean, ianomb-ean-a, pig-ian-a,
    KUTENDWAwsom-w-a
    KUTENDEWAew, iwomb-ew-a, pig-iw-a
    KUTENDEKAekpend-ek-a
    KUTENDESHAesh, ez, ish, izkom-esh-a, ing-iz-a
    KUTENDANAanfiny-an-a

    Aina za minyambuliko/kauli za vitenzi

    • Kutenda

    Hali ya kawaida ya kitenzi.

    • Kutendatenda

    Hali ya kitenzi kurudiwa.

    • Kutendea
      • Kwa niaba ya
      • Badala ya
      • Sababu
      • Kuonyesha kitumizi
      • Mwendo wa kitu kuelekea kingine
    • Kutendwa 
    • Huonyesha nomino iliyoathiriwa na kitenzi. 
    • Kutendewa
    • Humaanisha kitendo kimetendwa na mtu badala au kwa niaba ya mtu mwingine.
    • Kutendana
    • Unamtenda mtu jambo naye anakutenda jambo lilo hilo.
    • Kutendeana
    • Unamtendea mtu jambo naye anakutendea jambo lilo hilo.
    • Kutendeka
    • Uwezekano wa kitendo kufanyika
    • Kutendesha
    • Mtu au kitu kusababisha kufanyika kwa kitendo.
    • Kutendeshea
    • Kusababisha kitendo kitendeke kwa niaba ya mwingine.
    • Kutendeshwa 
    • Kusababishwa kufanya jambo.
    • Kutendeshewa
    • Mtu kusababishwa kitendo kitendeke kwa niaba yake.
      • Kutendeshana
    • Kusababisha kitendo kitendeke kwa mtu naye anasababisha kitendo kicho hicho kitendeke kwako.
      • Kutendesheana
    • Kusababisha kitendo kitendeke kwa niaba ya mtu naye anasababisha kitendo kicho hicho kitendeke kwa niaba yako.
      • Kutendesheka
    • Kitendo fulani kinaweza kusaababishwa.
      • Kutendama
    • Kuwa katika hali fulani bila ya mabadiliko.
    • lala-lalama
    • ficha-fichama
    • shika-shikama
    • ganda-gandama
    • chuta-chutama
    • funga-fungama
    • kwaa-kwama
    • unga-ungama
    • andaa-andama
    • saki-sakama
    • Kutendata
    • Hali ya mgusano au kushikanisha vitu viwili.
    • paka-pakata
    • fumba-fumbata
    • kokoa-kokota
    • okoa-okota
    • kama-kamata
    • Kutendua
    • Hali ya kiyume
    • choma-chomoa
    • funga-fungua
    • Kutenduka
    • Kuweza kufanyika kwa hali ya kinyume.
    • chomoka
    • funguka

Leave a Reply

scroll to top