Nomino katika ngeli hii huchukua kiambishi cha umoja LI na cha wingi YA ili kuleta upatanisho wa kisarufi.Huwa na majina ya sehemu za mwili, dhana, vifaa, nomino zilizo katika hali ya ukubwa n.k. Mifano ya nomino zipatikanazo katika ngeli hii ni;

  • jicho-macho
  • jina-majina
  • jitu-majitu
  • goma-magoma
  • jambo-mambo
  • janga-majanga
  • jembe-majembe
  • jeneza-majeneza
  • wazo-mawazo 
  • tunda-matunda
  • jua-majua
  • ziwa-maziwa
  • ua-maua
UmojaWingi
Dirisha limefunguliwaMadirisha yamefunguliwa
Jiwe limevunjikaMawe yamevunjika
Gari limeegeshwa kando ya barabaraMagari yameegeshwa kando ya barabara
Dege limepaaMadege yamepaa
Miundo ya nomino za Ngeli ya LI – YA
Nomino za ngeli hii huchukua miundo tofauti tofauti katika hali ya umoja na wingi;
JI- MA kwa mfano jifya – mafya
JA- MA kwa mfano Jani – Majani
JI – ME kwa mfano Jino- Meno
MA – Mashati, madege n.k.
Ngeli za Nomino
Ngeli ya A-WA
Ngeli ya U-I
Ngeli ya U-ZI
Ngeli ya YA-YA
Ngeli ya I-I
Ngeli ya U-U
Ngeli ya U-YA
Ngeli ya KI-VI
Ngeli ya KU-KU
Ngeli ya I-ZI
Ngeli ya PA-KU-MU