Shamirisho ala

Shamirisho ala /kitumizi. 

Huonyesha kile ambacho husaidia kutendeka kwa jambo au kitendo fulani katika sentensi.Ni kifaa ambacho hutumika, Mfano :

Mama anampikia mtoto chakula kwa sufuria, Kibarua alimlimia mkulima shamba kwa jembe.

Katika sentensi hizi mbili, sufuria na jembe ni Shamirisho ala au kitumizi.

        Mifano Zaidi

  • Mama alimpikia baba chakula kwa sufuria.
  • Baba alipikiwa chakula na mama kwa sufuria.
  • Sufuria ilitumiwa na mama kumpikia baba chakula.
  1. Chakula (Shamirisho Kipozi/Yambwa Tendwa)
  2. Baba (Shamirisho Kitondo/Yambwa atendewa)
  3. Sufuria (Shamirisho Ala/Yambwa Kitumizi)
Shamirisho
Shamirisho kipozi /yambwa tendwa. ( direct object)
Shamirisho kitondo /Yambwa tendewa. (indirect object)

Leave a Reply

scroll to top