SIFA MAJUMUI ZA LUGHA KATIKA FONOLOJIA

 SIFA MAJUMUI ZA LUGHA KATIKA FONOLOJIA

Madhumuni makubwa ya fonolojia ni kuweka wazi baadhi ya sifa majumui zinazojitokeza katika lugha asilia. Hii inatokana na ukweli kwamba kuna tofauti za wazi zinazojitokeza katika fonolojia ya mifumo mbalimbali ya lugha asilia, bado kuna sifa fulani ambazo zinaelekea kuchangiwa na lugha zote. Sifa zinazoelekea kuchangiwa na lugha zote asilia ndizo zinazoitwa sifa majumui za lugha.

AINA ZA SIFA MAJUMUI ZA LUGHA

(a)   SIFA MAJUMUI HALISI ZA LUGHA

Hizi ni zile sifa za kiisimu ambazo ni za kawaida katika lugha zote za binadamu. Kwa mfano, lugha zote za binadamu huwa na irabu na konsonanti katika orodha ya sauti zake; ingawa idadi ya irabu na konsonanti hizo huweza kutofautiana toka lugha moja hadi lugha nyingine. Vilevile, lugha zote asilia zina silabi, ingawa muundo wa silabi unaweza kutofautiana toka lugha moja hadi lugha nyingine; katika lugha zote asilia irabu na konsonanti hupangiliwa katika silabi.

(b)   SIFA MAJUMUI PANA ZA LUGHA

Hizi ni zile sifa ambazo hupatikana katika lugha nyingi, ingawa sio zote. Kwa mfano, wanaisimu wengi hukubaliana kwamba lugha nyingi za binadamu huwa zina angalau irabu tano. Pamoja na huo ukweli kuna ukweli mwingine kwamba kuna baadhi ya lugha chache ambazo zina irabu saba au zaidi, na kuna lugha nyingine zenye irabu tatu.

(c)    SIFA MAJUMUI TABIRIFU ZA LUGHA

Hizi ni zile sifa ambazo kuwapo kwa sifa moja ya msingi huashiria kuwepo kwa sifa nyingine ambayo inahusiana na hiyo sifa ya msingi. Kwa mfano ikiwa katika lugha kuna tonijuu basi kutakuwa na tonichini pia.

hati miliki zimehifadhiwa

Leave a Reply

scroll to top