Sifa za Kishazi tegemezi

Sifa za kishazi tegemezi

                    i.            Hakikamilishi taarifa pasipokuwepo na kishazi huru

Mfano;       Mtoto anayecheza mpira ameumia

                  Mvulana aliyefaulu mtihani amefurahi

                  Mama alipomkaribisha aliingia ndani

                  ii.            Kinaweza kuondolewa katika tungo bila kuathiri taarifa kusudiwa.

Mfano;      mtoto aliyeugua amepona

                  Mtoto amepona

                  Mama uliyemsalimia pale ameondoka jana.

                  Mama ameondoka jana

                iii.            Hutambulishwa na vitambulishi vya urejeshi vinavyopachikwa katika vitenzi.

Mfano; Anayesoma, Alichookota, Uliokatika, Iliyoibiwa, Alipoingia n.k.

                iv.            Vilevile kashazi tegemezi hutambulishwa na viunganishi tegemezi kwamba, ili, ili kwamba, kwa sababu, mzizi wa amba na kiambishi cha masharti.

Mfano;       Mama alisema kwamba motto ameumia

                  Mvulana ambaye ni kaka yangu amerejea nyumbani

                  Akijua atanichapa

Kishazi
Kishazi huru
Kishazi tegemezi
Aina ya vishazi tegemezi

Leave a Reply

scroll to top