SILABI

 Ni dhana ya kifonolojia ambayo huwakilisha umbo la matamshi ambapo sauti moja au zaidi hutamkwa kwa mara moja kama fungu moja.

Silabi ni kipashio cha kifonolojia ambacho ni kikubwa kuliko fonimu lakini kidogo kuliko neno katika mfumo wa darajia.

AINA ZA SILABI

1. SILABI HURU/WAZI

Ni silabi ambazo mara nyingi huishia na irabu. Msikiko wake ni mkiubwa.

SILABI FUNGE

Ni silabi ambazo huishia na konsonanti. Msikiko wake ni hafifu. Aghalabu irabu huchukuliwa kama kilele cha silabi. Aidha, irabu ni vitamkwa ambavyo vikitolewa hakuwi na mzuio wa hewa.

hati miliki zimehifadhiwa

Leave a Reply

scroll to top