Tofauti kati ya fonetiki na fonolojia

 ► Fonolojia inategemea uchunguzi uliofanywa na fonetiki wakati fonetiki haitegemei sana fonolojia.

► Fonetiki inachunguza sauti kama zilivyo.

► Fonolojia inachunguza sauti na maathiriano katika lugha fulani.

► Fonetiki ina seti kubwa ya sauti wakati fonolojia ina seti ndogo ya sauti ambayo ni sehemu ya seti ya fonetiki.

► Seti ya fonolojia ina kikomo wakati seti ya fonetiki haina kikomo. Inasemekana kuwa lugha nyingi duniani hutumia wastani wa sauti kati ya ishirini na arobaini tu. Kwa mfano lugha ya Kiswahili ina sauti 31.

► Fonetiki ipo moja lakini fonolojia ni nyingi  kama lugha zilivyo nyingi. Hivyo kila lugha ina fonolojia yake ambayo ni tofauti na fonolojia ya lugha nyingine

► Kipashio cha msingi katika fonetiki ni FONI wakati katika fonolojia ni FONIMU.

► Katika fonetiki sifa bainifu za foni hubainishwa wakati katika fonolojia tunabainisha sifa bainifu za FONIMU.

● Kwa ujumla fonetiki na fonolojia hutegemeana na kukamilishana.Uchunguzi na uchambuzi wa kifonetiki husaidia sana uchambuzi wa kifonolojia na vilevile uchambuzi wa kifonolojia husaidia uchambuzi wa kifonetiki. Hata hivyo fonetiki ni msingi imara ambao husaidia katika uchambuzi wa kifonolojia. Kwa upande mwingine fonetiki huzipata foni zote kutoka lugha mbalimbali, yaani kutoka fonolojia za lugha mbalimbali. Kwa maneno mengine tunaweza kusema kwamba kama hapangekuwepo hizo fonolojia za lugha mbalimbali basi wanafonetiki hawangekuwa na kitu cha kuchunguza.

hati miliki zimehifadhiwa

Leave a Reply

scroll to top