UKALIMANI NI NINI?

 Ukalimani imefasiliwa kuwa ni, uhusishaji wa kuhamisha maana kutoka lugha moja (lugha chanzi) kwenda lugha nyingine (lugha lengwa) katika mazungumzo. Hivyo basi tunaweza kusema pia, ukalimani ni hali ya mtu kuhamisha mawazo ya kinachozungumzwa kutoka lugha moja kwenda lugha nyingine katika mazungumzo. Hii ina maana kuwa ukalimani ni lazima uhusishe pande mbili, upande wa kwanza sharti awepo mtu anayezungumza lugha fulani na upande mwingine kunakuwa na mtu ambaye anasikiliza hicho kinachozungumzwa na kuyarudia hayo yanayozungumzwa kwa kutumia lugha nyingine tofauti na ile iliyotumiwa na mazungumzaji wa kwanza.

Hivyo basi, ukiangalia, maana hiyo tuliyoiangalia utaona kuwa, ukalimani ni taaluma inayohusu mazungumzo wakati tafsiri yenyewe uhusu maanadishi, kwa maana hiyo huwa tunatafsiri maandishi kutoka lugha moja kwenda lugha nyingine na tunakalimani mazungumzo kutoka lugha moja kwenda lugha nyingine.

Ukalimani ulianza pale ambapo mataifa mbalimbali yenye kuzungumza lugha tofauti tofauti yalipoanza kuingiliana na kushirikiana katika shughuli mbalimbali za kijamii, kisiasa, kichumi na kiutamaduni, kwa mfano ujio wa wageni Afrika Mashariki kama vile Waarabu, Wajerumani na Waingereza ili waweze kuwasiliana na wenyeji wao waliambatana na watu ambao walikuwa wakiwatumia kama wakilamani wao.

Kwa sasa hivi ukalimani umekuwa kama taaluma muhimu, ukalimani unafanyika katika mahakama, kanisani, katika mikutano ya kimataifa, mahubiri ya kidini, n.k na kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia, kuna vifaa maalumu ambayo hutumika kukalimani mazungunzo kutoka lugha moja kwenda lugha nyingine, ambayo huvaliwa masikioni katika kumbi za mikutano. Na sasa ni taaluma inayofundishwa katika shule za sekondari na elimu ya juu kama ilivyo kwa tafsiri kutokana na umuhimu wake.

Mkalimani ni mtu muhumi sana katika kufanikisha mawasiliano kwa watu wanaotumia lugha mbili tofauti, au lugha inayotumika katika eneo hilo msikilizaji haielewi na haijui na ndiyo maana utakuta wakalimani wakihitajika mahakamni, mikutano ya kimataifa, katika mahubiri ya kidini au mahali popote pale ambapo wazungumzaji hawawezi kuelewana kwa kuwa wanatumia lugha tofauti.


MAREJEO

Cartford [1995] A linguistic Theory Translation

Mwansoko, H.J.M na wenzake [2006] Kitangulizi cha Tafsiri, Nadharia na

Mbinu.TUKI.Dar-es-salaam

Newmark, P [1982] Approaches to Translation, Oxford, Pergamon Press

Newmark, P [1988] A Text book of Translation, London, Prentice Hall.

Oxford University Press Dar-es-salaam

Semzaba, E [2006] Ngoswe, Penzi Kitovu cha Uzembe. The General Booksellers LTD.

D.S.M

TUKI [2002] Kamusi ya Kiswahili Sanifu. TUKI, Dar-es-salaam

TUKI [1985] Kiswahili, Jarida la Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili.

www.bakita.org.tz retrieved on Monday 04th July 2018

www.jim-mission.org.uk retrieved on Monday, 04th July 2018

www.ajol.inf retrieved on Monday, 04th July 2018

Vitabu vilivyotafsiriwa ambavyo vimetumika kama marejeo

Ayi Kwei Armah, Wema Hawajazaliwa, kimetafsiriwa na Abdilatif Abdalla

Ferdinand Oyono: House boy, Kimetafsiriwa na Raphael Khasao na Nathan Mwele.

William Shakespeare: Juliasi Kaizari: Kimetafsiria na Julius K. Nyerere

Mabepari wa Venisi: Kimetafsiriwa na Julius K. Nyerere

Hekaya za Abunuwasi: Kimetafsiriwa na Interterritorial Language Committee, East Africa

Alfu Lela Ulela: Kimetafsiriwa na Sir Richard Burton

Sir Rider Haggard: Mashimo ya Mfalme Suleiman


hati miliki zimehifadhiwa

Leave a Reply

scroll to top